Propellerads

Monday, September 19, 2016

mpoma

AJALI ZA MATUKIO YA MABASI WILAYANI BUTIAMA

PropelleradsPICHA ZA MATUKIO YA AJALI YA MABASI YA J4 EXPRESS NA MWANZA COACH ENEO LA SABASABA WILAYA YA BUTIAMA.

HIVI NDIVYO MABASI YALIVYOGONGANA ENEO LA SABASABA NA KUDAIWA KUSABABISHA VIFO VYA ZAIDI YA WATU WA 29 HADI SASA KWA MUJIBU WA TAARIFA ZA AWALI.


Inaelezwa kuwa ajali hiyo imehusisha magari matatu  na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 30 na majeruhi zaidi ya 70 katika eneo la Sabasaba wilayani Butiama.

Ajali hii imetokea majira ya saa 5 na nusu,Majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara.

Kufuatia ajali mbaya iliyohusisha magari matatu wilayani Butiama mkoani Mara Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya Butiama  Anjelina Mabula aliyezungumza na TBC muda mfupi uliopita amesema idadi ya watu waliopoteza maisha ni 38 hadi sasa huku majeruhi wakiwa ni 80.

Amesema ajali hiyo  imehusisha basi la AM Coach lenye namba za usajili  T736 AWJ likitoka Musoma kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi T677 CYC J4 Express likitoka Mwanza kwenda Tarime na gari jingine dogo aina ya Nissan Corola P332 KKT likitoka eneo la Sabasaba yote yalikutana kwenye mteremko yakitokea juu kwenda Darajani.

Katika hali ya kupishana kutokana na spidi yao hawakuweza kupishana yakagongana na wakati huo gari hilo dogo  lilipaki pembeni baada ya kuona hali tete nalo likagongwa kwa nyuma likasukumwa na kutumbukia mtoni.

Katika gari dogo kulikuwa na watu 8,wawili wamefariki dunia na majeruhi 36 kutoka kwenye mabasi  hayo mawili nao wamefariki na majeruhi 80 wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Mara.

KUPATA KAZI POPOTE NCHINI BONYEZA 'HAPA' CHINI. Propellerads

mpoma

About mpoma

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :