JE,WAZIJUA SIRI KUMI ZA NDOA...SOMA HAPA
JE,WAZIJUA SIRI KUMI ZA NDOA
1. KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAE ANA UDHAIFU WAKE
Mungu pekee ndio haana udhaifu, Kila ua waridi lina chimbuko lake.
2. KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAE ANA HISTORIA YAKE MBAYA
Hakuna mtu ambae ni malaika,epuka kuchunguza mambo ya mtu ya nyuma samehe na usahau.
3. KILA NDOA INA CHANGAMOTO ZAKE
Ndoa sio kitanda cha maua waridi yanayomeremeta kila muda,kila ndoa yenye mafanikio imepitia misukosuko mingi.
4. KILA NDOA INA HATUA ZAKE KATIKA MAFANIKIO
Hatuwezi kuwa sawa, kuna watakaokuwa mbele kidogo na watakaokuwa nyuma kidogo. Kupunguza stress, kuwa mtulivu, fanya kazi kwa bidii na kwa muda muafaka ndoto za ndoa yako zitatimia.
5. KUOA AU KUOLEWA NI KUTANGAZA VITA
Ukishaoa au kuolewa ni kuingia katika uwanja wa mapambano,Kuwa tayari kupambana kuulinda ukanda wa ndoa yako.
6. HAKUNA NDOA ILIYOKAMILIKA
Hakuna ndoa ambayo imetimilika,Ndoa ni kazi ngumu,jitolee mwenyewe na ufanye kazi ya kuijenga ndoa yako iwe kamilifu.
7. MUNGU HAWEZI KUKUPA MTU KAMILI UNAYEMTAKA
Mungu atakupa mtu ili wewe umtengeneze jinsi wewe unavyohitaji yeye awe.
8. KUOA NI KUJIINGIZA KATIKA HATARI
Huwezi jua nini kitatokea baada ya ndoa, hali inaweza badilika,hivyo achia nafasi ya marekebisho.
9. NDOA SIO MKATABA WA MUDA BALI NI MKATABA WA KUDUMU
Ndoa inahitaji ahadi ya kudumu,mapenzi ni gundi ambayo huwafanya wanandoa kuwa pamoja daima..Talaka huanza katika mawazo.
10. KILA NDOA HUHITAJI KUJITOA
Hakuna mapenzi rahisi katika ndoa,huwezi kupenda au kupendwa bila kujitoa nafsi yako kwa dhati.
Vijana karibuni sana katika familia za wanandoa ila unatakiwa utoe uoga