Propellerads

Monday, December 26, 2016

mpoma

MATUKIO YA MKESHA NA SIKUKUU

Propellerads

MATUKIO YA MKESHA NA SIKUKUU YA KRISMAS DAR


Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania (KKKT) Alex Malasusa (katikati) akiendesha Ibada ya Sikukuu ya Krismasi iliyofanyika katika Kanisa la Azania Front Dar es Salaam leo asubuhi.Waumini wa Kanisa hilo, wakiwa kwenye ibada ya Sikukuu ya Krismas katika Kanisa la Azania Front leo asubuhi.



Azania Front...
Wakazi wa jijini Dar es Salaam wakitoka kwenye Ibada ya Sikukuu ya Krismas, iliyofanyika kwenye Kanisa la Azania Front leo.Askofu wa Kanisa la Menonite, Stephen Mang’ana, akiendesha Ibada ya Kitaifa ya Sikukuu ya Krismas, iliyosaliwa katika kanisa hilo leo asubuhi.
Waumini wa Dini ya Kikristu, wakiwa katika Ibada ya Sikukuu ya Krismas iliyosaliwa Kitaifa kwenye Kanisa la Menonite leo asubuhi. 
Wasanii wa kikundi cha Kwaya cha Kanisa la Tegeta jijini Dar es Salaam, wakiimba wakati wa Ibada ya Kitaifa ya Sikukuu ya Krismas, iliyofanyika kwenye Kanisa la Menonite leo.
Waumini wa Dhehebu la Anglikana, wakiwa katika Ibada ya Sikukuu ya Krismas iliyofanyika kwenye Kanisa la Mtakatifu Albano leo asubuhi.
Waumini wa Dini ya Kikristu wakiwa katika Ibada ya pili ya Sikukuu ya Krismas, iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph leo asubuhi. 
Waumini wa Kanisa la Mtakatifu Joseph, wakimbeba binti ambaye hakuweza kufahamika jina lake, aliyeanguka wakati wa Ibada ya Sikukuu ya Krismas ndani ya kanisa hilo leo, kutokana na hali ya hewa iliyosababishwa na uwingi wa waumini wa waliohudhulia ibada hiyo. 
Askofu Msaidizi wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, usebio Nzigilwa, wakiwa na wasaidizi wake baada ya kumaliza ibada ya usiku ya mkesha wa Sikukuu ya Krismas kwenye Kanisa na Mtakatifu Joseph jana usiku.
MAMBO YA MTAANI KINONDONI USIKU WA MKESHA.
Hata watu kama hawa pia walikuwepo mtaani wakisaka riziki, hapa ni mtaa wa Kinondoni Muslim, mdada huyu aliyejistukia baada ya kuona mwanga wa flash ya kamera, alikuwa na Sufianimafoto akiwa mitaa hiyo akisubiria wateja wa mambo fulani, anashtuka na kuficha uso tayari zamani picha ishapigwa na gari linatimua, akabaki aaaagh!... 
Watoto wa Mtaani wakiuchapa usingizi katika bustani ya Barabara ya Kawawa eneo la Kinondoni Moroco jana usiku.
KUPATA KAZI POPOTE NCHINI BONYEZA 'HAPA' CHINI. Propellerads

mpoma

About mpoma

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :