Propellerads

Saturday, October 29, 2016

mpoma

watatu wapoteza maisha

Propellerads

Watu watatu wapoteza maisha kwa ajali ya gari wakati wakielekea katika harusi

Abiria watatu kati ya tisa waliokuwa wakisafiria gari aina ya Toyota Noah T.878 CZY wamefariki dunia baada ya gari hilo kuacha barabara na kupinduka katika kona maarufu ya Mohammed Trans nje kidogo ya mji wa Singida.
Ajali hiyo ambayo pia imesababisha majeruhi watatu, abiria hao walikuwa wakitokea Dar es Salaam wakielekea Tabora kwa ajili ya kushehekea harusi ambayo ilipangwa kufanyika Ijumaa ya Oktoba, 29 kati ya Daniel Braisan Marangu na Lightness Godwin wote wakazi wa Bunju jijini Dar es Salaam.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, Mayala Towo, alisema ajali hiyo imetokea Oktoba, 27 majira ya saa mbili usiku katika kata ya Kindai tarafa ya Mungumaji barabara kuu ya Singida-Dodoma.
Aliwataja abiria waliopoteza maisha yao kuwa ni Lucas Alle Killo (26) muhitimu wa chuo kikuu Muhimbili na mkazi wa Boko,Tumaini Mwasongela (36) mfanyabishara mkazi wa Boko na Lilian Samwel Msuya (48) mfanyabiashara mkazi wa Mbezi,Dar es Salaam.
“Waliojeruhiwa ni Josephine Beda (28) mkulima mkazi wa Boko Bunju, Mpeli Bukuku (25) mkulima mkazi wa Kinondoni Mkwajuni na Anabela Jailos Sanga (32) mwalimu mkazi wa Bunju, Dar. Wamelazwa hospitali ya mkoani mjini hapa na hali zao zinaendelea vema,” alisema.
Kuhusu ajali hiyo, Towo alisema Noah hiyo mali ya mchungaji wa kanisa la Assemblies of God Basihaya Bunju, Dar, Michael Salaka, siku ya tukio lilikuwa linaendeshwa na Gidion Kamungisha (50) mkazi wa Boko Bunju, Dar.
Alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi uliopelekea dereva Kamungisha kushindwa kulimudu gari hilo.
“Kwa sasa tunamshikiria dereva Kamungisha kwa mahojiano na baada ya uchunguzi kukamilika,tuatamfikisha mahakamani kujibu tuhuma ya uzembe na kusababisha vifo,” alisema Kaimu kamanda huyo.
Alisema Jeshi la Polisi linatoa wito kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara kuwa waangalifu wawapo barabarani na kuendesha mwendo unaokubalika katika eneo hatarishi na kuchukua tahadhari zote wakati wa safari.
Eneo hilo la kona ya Mohammed Trans, limebatizwa jina hilo baada ya basi la kampuni hiyo ya jijini Mwanza kupinduka kwenye kona hiyo ya kuwaka moto ulioteketeza zaidi ya abiria 20 ambao wamezikwa kwenye kaburi moja kwenye eneo la kona hiyo.
KUPATA KAZI POPOTE NCHINI BONYEZA 'HAPA' CHINI. Propellerads

mpoma

About mpoma

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :